Mambo? Natumaini mnaendelea vizuri. Ningependa tuzungumze kidogo kuhusu wazo la faraja. Kwangu, inaonekana kwamba watu wote wako na jinsi yao ya kutafuta faraja wakati wanaipohitaji, na ningependa kujua jinsi yenu ya kuitafuta. Kwangu, wakati nasikia vibaya ama nahitaji faraja, napenda kuenda kupiga picha, ama kuangalia picha zangu za zamani. Pia, nikisikia vibaya kwa mwili, napenda kuenda kukimbia ama kuenda kwa baisikeli wakati nasikiliza musiki. Nikipigisha moyo wangu, najua nitasikia vizuri zaidi baadaye. Kusafisha chumba changu ni jinsi nyingine ya kupata faraja, kwa sababu siwezi kufikiri vizuri ikiwa naona fujo tu. Pia, napenda kuwapigia marafiki zangu simu ama kuenda kuwaona mkahawani ama nyumbani. Mimi ni mtu wa watu, kwa kweli. Napata mwanga kutoka watu wengine wakati ninaposikia nimezungushiwa na giza mimi. Hii ndio maana marafiki zangu ni muhimu sana: wananisaidia wakati ninapokuwa giza, na mimi najaribu kuwasaidia wakati wanapokuwa giza wao.
Najua lakini kwamba watu wengine hawapendi kuhitaji watu wengine kwa kupata faraja, na wangependelea kutafuta faraja kutoka wao wenyewe. Hawapendi kuhitaji mtu mwengine, labda kwa sababu wanaogopa yule ataondoka siku moja, na watakuwa peke yao. Hawapendi kutegemea na watu wengine.
Sijui ikiwa ningeweza kuendelea bila kutegemea na watu wengine, hata ikiwa ningependa kuijaribu. Na ninyi? Mnategemea na watu wengine, ama mnawapenda tu bila kuwategemea? Ikiwa mnategemea nao, mnafanya nini wakati hawapo? Ikiwa hamtegemea nao, mnafanya nini kwa kutafuta faraji (isipokuwa kuitafuta nao)?
Thursday, February 26, 2009
Subscribe to:
Posts (Atom)